Jumla ya malalamiko 78 ya vitendo vya rushwa Mkoani Katavi yameripotiwa katika taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa katika kipindi cha mwezi Julai 2017 hadi Machi 2018. Akitoa taarifa ya mwaka kwa Vyombo vya Habari Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Ndugu Christopher Lawrence Nakua amesema,taarifa zilizopokelewa zimeainisha Idara na Taasisi mbalimbali zilizotuhumiwa na vitendo vya Rushwa ikiwa ni Taasisi za serikali na Binafsi. Ambapo Halmashauri Kimkoa zina jumla ya malalamiko 78,Polisi malalamiko 6,Chama cha Ushirika malalamiko 2,Idara ya Afya malalamiko 6,Sekta binafsi (BAYPOT na PRIDE) malalamiko 2. Mashirika ya Umma (TANESCO na TARULA) malalamiko 3,Idara ya Elimu malalamiko 5,Idara ya Mifugo malalamiko 2,Idara ya Uvuvi lalamiko 1 na Ofisi ya Makazi ya Wakimbizi lalamiko 1. Aidha,Idara na Taasisi zingine zilizotajwa ni pamoja na uhamiaji lalamiko 1,Idara ya Ardhi malalamiko 5,Idara ya Ujenzi malalamiko 3,Serikali ya Vijiji malalamiko 10 na Sekta ya Madini lala...